Pages

Subscribe:

Sunday, 7 August 2016

DAWA KWA MATATIZO YA PRESHA

Kipimo cha kisasa cha matatizo ya presha
Ugonjwa wa Presha mara nyingi husababishwa na mambo yafutayo;
1. Msongo wa mawazo 2. Mafuta mengi mwilini 3.Matumizi ya ulevi 3. Kula chumvi nyingi n.k.
Hivyo kama wewe tayari unatatizo la ugonjwa wa presha kabla ya kutumia dawa zingatia mambo yafuatayo;
I) Punguza msongo wa mawazo kwa ☆ Kuwa bize na shughuli mbali mbali za kila siku ☆ Omba ushauri kwa mtu wa karibu yako unapokua na tatizo ☆ Jishughulishe na michezo. Mfano mpira wa miguu.
II) Punguza mafuta kwa kiasi kikubwa katika chakula unachokula hii ni pamoja na kuupatia mazoezi ya kutosha mwili wako.
III) Acha ulevi na tumia chumvi kwa uangalifu ndani ya chakula chako. 
Ukifanikiwa kua makini ndani ya mambo haya sasa unaweza kuandaa dawa yako kama ifuatavyo;

A) Ponda ponda vitunguu thaumu kwa wingi kisha tengeneza juisi kutokana na maji.
Vitunguu thaumu
MATUMIZI.
Kunywa juisi ya vitungu thaumu vijiko vya chakula 3 kutwa mara 3 kwa muda wa siku 21 hadi 30.
ANGALIZO: usitumie dawa hii kama wewe ni mgonjwa wa Sukari na unatumia Sindano au Vidonge vya Insulini badala yake tumia dawa B) hapo chini.
B) Ponda ponda vitunguu maji ili upate juisi yake bila kuchanganya na maji, changanya na asali kulingana na wingi wa juisi ya kitunguu maji mfano; Juisi ya vitunguu lita moja na asali lita moja.
Vitunguu maji
MATUMIZI.
Kunywa vijiko 3 vya chakulaku kutwa mara 3 kwa muda wa siku 21 mpaka 30.
NB:  Fuata hatua tulizo eleza hapo juu kwa matokeo mazuri na yaharaka zaidi

0 comments:

Post a Comment