STAA wa Soka wa Ufaransa
anayetarrajiwa kujiunga na Klabu ya Manchester United ya uingeeza
akitokea Juventus kwa uhamisho wa gharama kubwa zaidi kuwahi kutokea
duniani, akiwa ni miongoni mwa mashabiki wa ‘kufa mtu’ waliohudhuria
show ya mwanamuziki Drake kwenye ukumbi wa Madison Square Garden, jijini
New York, Marekani.
Pogba ambaye bado ni mchezaji wa
Juventus yupo mapumzikoni nchini Marekani. Kiungo huyo mwenye miaka 23
ambaye hivi karibuni atakamilisha usajili wa paundi zaidi ya milioni 100
kwenda Man United alienda nyuma ya jukwaa na kumkabidhi Drake jezi ya
Juve.
Drake alikuwa akitumbuiza kwenye show ya ziara yake, Summer Sixteen. “Thanks to my bro @champagnepapi for this crazy performance last night .. #legend ah Oui hein #summersixteen #ovo,” aliandika Pogba kwenye picha akiwa na Drake aliyoiweka Instagram.
Kwenye picha nyingine inayomuonesha Drake akichukua selfie na Pogba, mchezaji huyo ameandika: Very nice meeting you bro @champagnepapi #holidays.”
Naye Drake ameshare picha kwenye Instagram akiwa na staa huyo na kuandika : When @paulpogba comes to see you that’s a
Mchezaji huyo anaonekana kufurahia mapumziko yake Marekani.
0 comments:
Post a Comment