Pages

Subscribe:

Sunday, 7 August 2016

Rwanda na Burundi vitani Tena!


Nkurunzinza.jpg 
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza.
UHUSIANO baina ya Burundi na Rwanda umeingia tena shubiri baada ya serrikali ya Burundi kuyazuia mabasi ya abiria kutoka nchini mwao kwenda Rwanda.


Taarrifa zimeeleza kuwa, Burundi inaishutumu Rwanda kuwapa mafunzo waasi wanaotaka kuiangusha Serikali ya Rais Pierre Nkurunziza.
Waendeshaji wa huduma hiyo ya kusafiisha abiria kati ya nchi hizo mbili wamezuiwa na maofisa uhamiaji wa Buundi kwenye mipaka ambao wamekuwa wakiwataka abiria washuke kwenye mabasi na kupita mipakani kwa miguu huku mabasi yakizuiliwa kuvuka.
rwanda (5)Rais wa Rwanda, Paul Kagame.
Pierre Nkurikiye ambaye ni msemaji wa Jeshi la Polisi la Burundi amesema wanataka kuzuia aina yeyote ya usafirishaji wa chakula kutoka Burundi kwenda Rwanda.
Serikali ya Burundi imelaani vikali kitendo cha vikosi vya usalama vya Rwanda kutoa mafunzo ya kijeshi kwa waasi wanaotaka kupindua serikali ya rais Pierre Nkurunziza, wakati huko Rwanda imepuuzia madai hayo.

0 comments:

Post a Comment