UHUSIANO baina ya Burundi na
Rwanda umeingia tena shubiri baada ya serrikali ya Burundi kuyazuia
mabasi ya abiria kutoka nchini mwao kwenda Rwanda.
Taarrifa zimeeleza kuwa, Burundi inaishutumu Rwanda kuwapa mafunzo waasi wanaotaka kuiangusha Serikali ya Rais Pierre Nkurunziza.
Waendeshaji wa huduma hiyo ya kusafiisha
abiria kati ya nchi hizo mbili wamezuiwa na maofisa uhamiaji wa Buundi
kwenye mipaka ambao wamekuwa wakiwataka abiria washuke kwenye mabasi na
kupita mipakani kwa miguu huku mabasi yakizuiliwa kuvuka.
Pierre Nkurikiye ambaye ni msemaji wa
Jeshi la Polisi la Burundi amesema wanataka kuzuia aina yeyote ya
usafirishaji wa chakula kutoka Burundi kwenda Rwanda.
Serikali ya Burundi imelaani vikali kitendo cha vikosi vya usalama
vya Rwanda kutoa mafunzo ya kijeshi kwa waasi wanaotaka kupindua
serikali ya rais Pierre Nkurunziza, wakati huko Rwanda imepuuzia madai
hayo.
0 comments:
Post a Comment